Job 18:5-14


5 a“Taa ya mwovu imezimwa,
nao mwali wa moto wake umezimika.
6 bMwanga hemani mwake umekuwa giza;
taa iliyo karibu naye imezimika.
7 cNguvu za hatua zake zimedhoofishwa;
shauri lake baya litamwangusha.
8 dMiguu yake imemsukumia kwenye wavu,
naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
9 eTanzi litamkamata kwenye kisigino;
mtego utamshikilia kwa nguvu.
10 fKitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake;
mtego uko kwenye njia yake.
11 gVitisho vimemtia hofu kila upande,
na adui zake humwandama kila hatua.
12 hJanga linamwonea shauku;
maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
13 iNayo yatakula sehemu ya ngozi yake;
mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
14 jAtangʼolewa kutoka usalama wa hema lake,
na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
Copyright information for SwhNEN